Msanii wa kundi maarufu la P-Square, Peter Okoye kutoka Nigeria amethibitisha kuwepo kwa tofauti kati ya ndugu hao na meneja wao ambaye pia ni kaka yao mkubwa Jude Okoye.
Siku ya Jumanne (Feb 16) Peter alimwaga mvua ya tweets kueleza kuhusu kutofautiana na meneja wao na kuwatahadharisha watu wasifanye biashara yoyote na kaka yao kwani wao hawataitambua.
Jude Okoye amekuwa meneja wa kundi hilo toka lilipoanzishwa.
“Mahabiki wa P-Square najua mmekuwa mkiuliza maswali mengi kuhusu sisi, Sina tatizo lolote na Paul bali ni uongozi.” ilisomeka tweet moja ya Peter.
Katika tweet hizo Peter amesisitiza kuwa hawamtaki kaka yao Jude kuwa meneja tena wa kundi hilo na kuwa wanahitaji kuubadilisha uongozi mzima. Moja ya sababu aliyoitaja ni kutoridhishwa na uongozi huo aliodai unawaongoza bila kuwa na mfumo.
Pacha wa Peter, Paul Okoye na kaka yao mkubwa Jude Okoye hawajasema chochote hadi sasa kuhusiana na tweets za ndugu yao.
Tweet hizo zimesomeka hivi:
“Uaminifu wangu kwa PSquare na mashabiki utaendelea kubaki kwa asilimia 100.”
“Meneja anaajiriwa na msanii na sio kinyume na hivyo.”
“PSquare ni Peter na Paul Okoye.”
“Usher Raymond amewahi kufanya, Beyonce amewahi kufanya pia, hivyo sio kitu kipya.”
“Watu hubadili uongozi na hauna tofauti.”
“Peter na Paul wanahaki ya kuutimua uongozi mzima, biashara ni biashara. Basi.”
“Peter na Paul ni Psquare, na mtu mwingine yeyote ni kiambatanisho tu.”
“Tafadhali yeyote anayefanya malipo na Northside Entertainment au Jude Okoye kwa niaba ya PSquare ajue isi hatuhusiki.#Onyo”
“Biashara ya familia inaumiza sana”.
“Unawezaje kuendesha biashara bila kuwa na mfumo.”
“Nimewahi kujutia vitu vingi kwenye maisha yangu…lakini niamini hili sio moja wapo. #HakunaTenaBiasharaYaFamilia.”
“PSquare haivunjiki. Lakini uongozi lazima uondoke.”
Tweets by @PeterPsquare
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Author Details
Welcome to Bamba One Media, your trusted destination for timely, engaging, and wide-ranging content from across the globe. We go beyond just headlines, bringing you a complete media experience that keeps you informed, aware, and connected to what matters most.
At Bamba One Media, we cover it all. From hard news shaping the world, to the latest in entertainment and music, from fast-moving sports updates to insights in business and finance, and the innovations driving the future in technology, our platform is built to keep you ahead of the curve.
Behind the platform is a voice driven by passion and purpose: delivering fresh, relevant, and compelling stories every day. Whether it’s breaking news, rising artists, major sporting moments, market trends, or viral stories making waves online, we aim to bring clarity, perspective, and energy to every piece of content.
Bamba One Media isn’t just about staying informed; it’s about experiencing the world in real time.
Welcome to Bamba One Media - Your Daily Source for News, Culture, and Innovation.
Stay connected. Stay updated. Stay ahead.



No comments:
Post a Comment